Monday 14 April 2014

MCHANGO WA WANAFUNZI WA SHAHADA YA UTALII 2011-2013 (SUA) KATIKA KUKUZA UTALII WA NDANI.


        Leo kwenye makala yetu tunaangaza katika Utalii wa ndani. Jicho letu limeelekea mji kasoro bahari((Morogoro) katika Chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine
Sokoine University of Agriculture 





 
 Chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine ni chuo kinacho toa shahada za kilimo na nyinginezo lakini takribani miaka mitatu iliyo pita chuo hiki kilianzisha Shahada  ya Utalii.Ni kvipi basi shahada hii imesaidia kukuza utalii wa ndani?
     Wanafunzi wanaochukua Shahada ya Utalii wameonekana kuwa na muamko mkubwa wa kutembelea vivutio mbalimbali pamoja na Hifadhi za Taifa kama vile Mikumi, Kilimanjaro,Saadani, Lake Manyara na Mamlaka ya hifadhi za Ngorongoro,pia  wanafunzi hao wameweza kutembelea vivutio  vingine kama vile Kaole na Ngome Kongwe huko Bagamoyo,Mapango ya Amboni pamoja na Fukwe za Ushongo zilizopo Tanga.
  Hali kadhalika wanafunzi hao hawakukosa kuwa wazalendo pia wameweza kutembelea vivutio vilivyopo katika mji wa Morogoro zikiwemo Uluguru Nature Reserve na Udzugwa Nature Reserve.Hata hivvo basi wanafunzi wachache wa mwaka wa masomo 2010-2013 waliweza kuanzisha chombo kinachoandaa trip mbalimbali kilichojulikana kama Domestic Tourism Promoters (DOTOPs).


Kilimanjaro at Uhuru peak
 Lake Manyaral













Ngorongoro conservation area
Kaole

Picha ya pamoja kaole0








0
Uluguru nature conservation














   Hivyo basi Wanafunzi wa Shahada ya Utalii wamekuwa chachu katika kukuza utalii wa ndani  kwa wakuweza kuwashawi wanafunzi wa Shahada nyingine kama vile Shahada ya Elimu na Maendeleo ya Vijiji kuwa na hari  ya kutembelea vivutio vya Utalii

Thursday 10 April 2014

" ZITUMIKE NJIA MBADALA KUKOMESHA UJANGILI"

Meno ya ndovu yakiteketezwa
   Kamati Tendaji Umoja wa Wabunge  wa Uhifadhi na matumizi Endelevu ya wanyamapori,imebaini Tanzania inapaswa kutumia njia tatu mbadala zitakazodhibiti ujangili.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kamati hiyo Riziki Lulinda,maazimio hayo yametokana na kikao  cha kamati hiyo kilichoketi Mjini Dodoma kuchambua sheria ya Uhifadhi Wanyamapori ya mwaka 2009.
  Alisema wamebani upungufu karika sera ya uhifadhi wa wanyamapori kwamba serikali  imeshindwa kuonyesha  namna itakavyoshirikiana na wananchi wanaoishi katika   maeneo yenye  hifadhi na yanayozunguka mapori ya Akiba  katika majukumu ya uhifadhi. Alisema wananchi hawajapewa elimu sahihi  inayoonesha umuhimu wa wanyamapori kwa uchumi wao na Taifa na sera imeshindwa kuonyesha mbinu na mikakati au mipango ya kuondoa au kupunguza ugomvi kati ya wafugaji , wakulima na hifadhi za Taifa.
   Alisema Taifa linapaswa kudhibiti masoko yanayotumika kwa biashara haramu ya nyara za Taifa na kudhibiti uwindaji haramu katika hifadhi. 
“Katika uchambuzi wa tatizo la msingi  la ujangili hapa nchini kamati imebaini kuwa ujangili ni sawa na mchezo wa paka na panya “, alisema  Lulinda.Alisema kufikia mkakati  wa kukabiliana  na tatizo la ujangili nchini kamati  ilibaini  kuwa kama Taifa tunaitaji kuainisha  maeneo tunayowaza kuwaona au kuwapata majangili na ili kufanikisha hilo tunahitaji wataalamu  wa uchunguzi.
 
 “Iwapo ili litafanyika  wananchi watashiriki kuonyesha  maeneo wanayojificha majangili na hii ni kwasababu majangili huhitaji msaada wa wananchi kupata  silaha, chakula , maji na zana nyingine za kufanikisha ujangili” Aisema Riziki. 

Saturday 5 April 2014

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni Mahali pekee panapohifadhi wanyamapori na binadamu

Ziwa Magadi
Ngorongoro:
Ni  eneo pekee panapohifadhi wanyamapori na binadamu, mchanga unaohama, palipogunduliwa nyayo za miguu na fuvu la binadamu wa kwanza.
Pia, kuna Ziwa Magadi ndani ya bonde refu na kubwa maarufu kwa jina la ‘Ngorongoro Crater’ lililosababishwa na milipuko ya volcano zaidi ya miaka 2000 iliyopita.
Mahali hapo si pengine popote, ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (Ngorongoro Conservation Area Authority – NCAA) iliyoanzishwa mwaka 1959 na kukabidhiwa majukumu makuu yafuatayo:
Kuhifadhi maliasili (wanyamapori, ndege na mazingira) zilizopo, kuendeleza binadamu wenyeji (Wamaasai) na utalii katika hifadhi hiyo.

Ina eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 8,292, inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) upande wa Kaskazini Magharibi na miji ya Arusha, Moshi na Mlima Kilimanjaro upande wa Mashariki.

Thursday 3 April 2014

MBINU MBALIMBAL ZITUMIKE KUKUZA UTALII WA NDANI.

Watalii wa ndani
Pamoja na mbinu  mbalimbali zinazotumika katika kuvitangaza vivutio na hifadhi zetu hapa nchini, utayari wa wananchi umekuwa ni mdogo katika kutembelea vivutio hivyo.Hivyo basi huu ndio muda muafaka wa wananchi na watu maarufu  kutembelea hifadhi na vivutio tulivyonavyo,i.li kukuza utalii wa ndani.
Watu maarufu kama wanasiasa, viongozi wa dini serikali wanamichezo, wasanii wa muziki na tamthilia wanao uwezo wa kuvitangaza zaidi vivutio vyetu kwa wananchi kutokana na utembeleaji wao.Vivutio ni pamoja na hifadhi za Taifa kama vile Mlima Kilimajaro,Tarangire,Saadani,Mkomazi na nyinginezo.

Sunday 30 March 2014

Intoduction....!

Hello.
 
Makundi ya wanyamapori
Wadau wangu napenda kuwakaribisha kwenye block mpya ya Utalii inayofahamika kama Tourism and Leisure Blog kujionea vivutio mbalimmali vinavyopatikana nchini kwetu (Tanzania).