Sunday 22 November 2015

HIFADHI YA MKOMAZI NI KIVUTIO KIZURI NCHINI TANZANIA



Hifadhi ya Mkomazi ipo katika mikoa miwili ambayo ni Kilimanjaro na Tanga, ndani ya wilaya za Same na Lushoto nchini Tanzania. Hifadhi ya Mkomazi ilianzishwa mnamo mwaka 1951 kama Pori la Akiba lilitengwa kutoka katika Pori kubwa la Akiba la Ruvu.
 Hifadhi hii ina ukubwa wa kilometa za mraba .Pori hili lilipendekezwa kuwa hifadhi ya taifa kwa misingi ya kunusuru maeneo na rasilimali zilizomo kutokana na matumizi yasiyoendana na uhifadhi kwa ajili ya kizazi cha leo na kijacho.
Katika hifadhi hii kuna wanyama na ndege wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na mbwa pori na vifaru weusi walioingizwa kutoka kutoka nchi ya Afrika kusini

No comments: