Tuesday 3 November 2015

MAKUMBUSHO YA TAIFA YA VIUMBE HAI YA ARUSHA


ADVERTISE WITH US CALL..0653683428


Ni moja ya makumbusho zinazopatikana katikati ya jiji la Arusha inayopatikana barabara ya Boma karibu na ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa AICC, ofisi za Manispaa pamoja na ofisi za Mkoa Arusha. Makumbusho ipo kwenye Boma iliyojengwa na Wajerumani katika miaka 1900 iliyokuwa ikitumika kama jengo la Utawala na mawasiliano wakatiki wa ukoloni wa Kijerumani

Makumbusho ilifunguliwa rasmi mnamo mwaka 1987 na kuonesha historia ya binadamu wa kale, ikiwepo pamoja na tafiti zilizofanyika katika bonde maarufu la Olduvai na alama za za miguu wa binadamu wa kale za Laetoli. Pia inafanya Maonyesho juu ya entomolojia ambayo huwasilisha baadhi ya wadudu, ndege na wanyama pamoja na umuhimu wao kiuchumi ambacho pia ni kivutio kikubwa kwa wageni wanaotembelea makumbusho hii.

 Advertise with us....call 0653683428

No comments: